IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Mashindano ya Qur’ani yakamilika huko Andhra Pradesh nchini India

21:51 - February 12, 2024
Habari ID: 3478340
IQNA - Mashindano ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu yalifanyika Vijayawada, Jimbo la Andhra Pradesh nchini India.

Closing ceremony of a Quran competition in India’s Andhra Pradesh

Mashindano ya 9 ya Kuhifadhi Qur'ani, yaliyoandaliwa na Jukwaa la Umoja wa Mafunzo ya Qur'ani, yalimalizika Jumapili.

Tukio hilo lilionyesha vipaji vya washiriki waliosoma aya kutoka kwa Surah Ar-Rahman, kwa kuzingatia sheria za Tajweed. Mashindano hayo yalilenga kuhifadhi turathi za kitamaduni, kuimarisha ujuzi wa kuhifadhi, na kukuza ujuzi wa Qur’ani

Tukio hilo lililofanyika chini ya uangalizi wa Mohammad Dawood, mwenyekiti wa kongamano hilo, liliwaleta pamoja washiriki wa rika na tabaka mbalimbali za maisha, wote wakiwa wameunganishwa kwa heshima yao kwa Qur’ani Tukufu

Shindano hilo lililochukua siku kadhaa, liligawanywa katika vikundi vinne tofauti, kila kimoja kikionyesha vipaji vya watu binafsi kuanzia watoto hadi watu wazima. Washiriki walipewa muda usiozidi dakika tatu kusoma aya za kutoka kwa Surah Ar-Rahman, sura inayosifika kwa uzuri wake wa kishairi na hekima ya kina.

Kwa kuanzisha masomo ya Qur’ani kwa watoto na vijana wazima, Dawood alionyesha matumaini kwamba vizazi vijavyo vitaongozwa na mafundisho ya Qur’ani Tukufu, na hivyo kudumisha dhamira thabiti ya uchamungu na hekima.

3487156

captcha