Amesema Aghalabu ya mahujaji wa kigeni, yaani zaidi ya 1,631,000 wamewasilia nchini humo kwa ndege huku waliosalia wakiwasilia kwa nchi kavu au bahari.
Kwa mujibu wa Idara ya Hija Saudi Arabia, Indonesia ndio nchi yenye idadi kubwa zaidi ya Mahujaji mwaka huu wa 1438 Hijria sawa na 2017 Miladia. Inatazamiwa kuwa Waindonesia 221,000 watatekeleza ibada ya Hija mwaka huu. Indoneisa iko Kuisni Mashariki mwa Asia na ina idadi ya watu milioni 261 na hivyo kuifanya kuwa nchi ya Kiislamu yenye idadi kubwa zaidi ya watu duniani. Nchi zingine zenye idadi kubwa ya Mahujaji ni Pakistan (179,210), India (170,000), Bangladesh (128,000), Nigeria (95,000) na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (86,500).
Mahujaji kutoka nchi za kigeni na wanaoishi ndani ya Saudia mwaka huu wanakadiriwa kuwa milioni mbili.